Anerlisa wa Ben Pol "Namkubali Sana Harmonize Alitaka Kuwekeza Kwangu"



“Ommy Dimpoz ni rafiki yangu, Harmonize alitaka kufanya biashara na mimi, Ali Kiba ni rafiki yangu kabla hata ya Ben Pol, wote hao nilikuwa nawasiliana nao hata wakati nipo kwenye ndoa.

“@harmonize_tz alitaka kuwa balozi kwenye biashara zangu, siwezi kuzungumza mambo mengi kwa kuwa Harmonize ni mtu wa kuweka mambo yake kwa siri.

“Wanasanii ninaowakubali wa Tanzania ni #Harmonize, Ali Kiba, Goodluck, Marioo, Nandy, na Mbossi.”

Hizo ni kauli za aliyewahi kuwa mke wa Msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol aitwae Anerlisa ambaye amewasili Dar es Salaam, leo Ijumaa, amezungumza hayo alipokuwa Uwanja wa Ndege (JNIA).

Alipoulizwa kuhusu kupunguza unene ikidaiwa alifanyiwa upasuaji wa kupunguza mwili, alisema: “Sijufanya upasuaji, kupunguza mwili ni kitu cha kawaida, nilifanya mazoezi tu na kula vizuri.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad