Man United wasukwa upya, wapiga Villareal 2-0 kwenye UEFA bila kocha





United walifuzu kuingia duru ya 16 baada ya kusajili ushindi wa 2-0 dhidi ya Villarreal nchini Uhispania
Cristiano Ronaldo na Jadon Sancho ndio walifunga mabao hayo yaliyosaidia Mashetani Wekundu kusajili ushindi katika mechi yao ya kwanza bila kufunzwa na Solskjaer
United watakuwa viongozi katika kundi lao iwapo Atalanta watashindwa kupiga Young Boys
Manchester United wamefuzu kuingia katika raundi ya muondoano ya mchuano wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Villareal katika mechi yao ya kwanza tangu kuondoka kwa Ole Gunnar Solskjaer.

Man United Wapata Msisimko Mpya, Wapiga Villareal Bila Kunolewa na Kocha
Cristiano Ronaldo na Jadon Sancho ndio walifunga mabao hayo yaliyosaidia Mashetani Wekundu kusajili ushindi. Picha: Eric Alonso.
Chini ya uongozi wa kaimu kocha Michael Carrick, United walifaulu kuwapiga vijana wa Unai Emery katiak mchezo ambao huenda wangelitoka droo.

Cristiano Ronaldo ndiye alibeba timu hiyo kutwaa ushindi katika dakika ya 78 na kuongezea jumla ya magoli yake kuwa 140.


Kisha Jadon Sancho alipiga msumari wa mwisho katika jeneza la Villareal dakika za lala salama na kuwa bao lake la kwanza na Manchester United.


 
Victor Wanyama Aongoza Montreal Impact Kushinda Kombe la Canada
Katika mechi hiyo, Carrick alifanya mabadiliko kadhaa akimshirikisha Donny Van de Beek katika timu ya kwanza naye XI akichukuwa nafasi ya Bruno Fernandes.

United walichechemea katika dakika za kwanza za mchezo huo huku Villareal wakitawala kila idara huku uwoga ukionekana kuwavaa Mashetani Wekundu.

United walihangaika kwenye safu ya mashambulizi, Cristiano Ronaldo akijipata kila mara ametengwa na kuwa na mwanya kati yake na Anthony Martial.


Carrick aliwatambulisha Bruno Fernandes na Marcus Rashford katika kipindi cha pili na kuongezea ubunifu huku Van de Beek na Martial wakipumzishwa.

United wana kila sababu kumshukuru mlinda lango David De Gea, ambaye alikuwa na kibarua kikubwa kupangua makombora ya Manu Trigueros.

Baada ya ukombozi huo, dakika 12 mechi hiyo kukamilika, kiungo wa kati wa United Fred alichuma nafuu kutokana na masihara ya Villareal akimumegea pasi Cristiano Ronaldo ambaye alipachika mpira wavuni na kumwacha hoi Geronimo Rulli ambaye alikuwa amezubaa.

Juhudi za Jadon Sancho, hatimaye zilizaa matunda baada ya mashambulizi kumshuhudia nyota huyo wa zamani wa Borussia Dortmund akipokea mpira kwenye kisanduku na kufunga bao lililowapa ushindi wenyeji wa Old Trafford.


 
Kocha Ole Gunnar Amwaga Machozi Baada ya Kupigwa Kalamu na Man United
United watakuwa viongozi katika kundi lao iwapo Atalanta watashindwa kupiga Young Boys.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad