Mkuu wa Wilaya Alipishwa Faini Baada ya Kugonga Kifaranga Cha Kuku


Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Paul Chacha alilazimika kusimamisha Msafara baada ya Dereva wake Alfred Chaki kugonga Kifaranga katika Kijiji cha Makingi alipokuwa anaendelea na ziara ya ukaguzi wa miradi ya mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Uviko-19.

Mkuu huyo wa Wilaya alimuamuru dereva wake alipe fidia ya Shilingi "Elfu Tano" na alikemea tabia ya Madereva kugonga Kuku, Bata, Kanga au Mnyama wa aina yeyote na kisha kuondoka.

Aidha, alisisitiza wananchi walime na kufuga kisasa ili wajikwamue kiuchumi

Mkuu wa Wilaya Chacha pia aliwaomba radhi akina Mama waliokuwa eneo la tukio na walimshukuru na kumpa baraka za kuendelea na Safari.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad