Simba Yaipiga 3-0 Red Arrows, Morrison Ang'ara Usipime



TIMU ya Simba ya Tanzania imeibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Red Arrows ya Zambia katikap Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo, umepigwa leo Jumapili, tarehe 28 Novemba 2021, kuwania kuingia hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika huku ikishuhudia Red Arrows mchezaji wake akipigwa kandi nyekundi.

Ni mchezo ambao umeshuhudia Bernard Morrison akicheza kadanda safi na lenye kuvutia kwa kufunga magoli mawili, kutoa pasi ya goli pamoja na kukosa mkwaju wa penati.

Dakika 90 zimemalizika kati ya 180 ambapo, tarehe 5 Desemba 2021, Simba watasafri kwenda Zambia kwee mchezo wa marejeo na kuhitmisha dakika zingine 90.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad