Walimu wa Chuo Kikuu Abuja Watekwa Pamoja na Watoto wao




Taarifa kutoka Nigeria zinasema wanaume wenye silaha wamekivamia chuo kikuu cha Abuja, kilichopo mji mkuu wa nchi hiyo.

Wakazi wa chuo ambao hawakutaka majina yao kutajwa , wamethibitisha shambulio hilo katika eneo la chuo la Gwagwalada, kutokea majira ya saa saba usiku wa nchi hiyo.

Download Our Udaku Special APP Kutoka Google Play Store Kwa Kutumia Link Hii Hapa>>>

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwalimu mmoja, ni kuwa walimu watatu na watoto wao wawili walichukuliwa mateka.

Taarifa zinasema wanaume hao wenye silaha waliwashinda nguvu walinzi wa chuo na kuweza kuingia katika nyumba za walimu na kuwateka.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad