Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene amewataka wote wanao tamani kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka kwa kutumia magari yao binafsi, kuhakikisha wanayafanyia uchunguzi wa kina na wa kitaalamu kabla ya kuyatumia.
Waziri Simbachawene ametoa kauli hiyo akiwa Jijini Arusha alipotembelea karakana ya ufundi wa magari Chuo Cha Ufundi Arusha ambapo amesisitiza kuwa hatua hivyo itasaidia kuepusha ajali za barabarani zisizo za lazima.
Aidha amewakumbusha madereva wote wa vyombo vya usafiri wa umma, kuhakikisha wanazingatia sheria za barabarani wakati wote wanapokuwa barabarani. ''Katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ni muhimu kuzingatia sheria za barabarani''.