Askari Polisi Aliyesifia Gongo Atimuliwa Kazi




Konstebo wa Polisi, Ramadhani Khalfan Said amefukuzwa kazi kwa kwenda kinyume na mwenendo mema wa Jeshi la Polisi Tanzania baada ya kunaswa kwenye mkanda wa video akisifia pombe haramu aina ya gongo huku akiwa amevalia sare za jeshi hilo.

Imeelezwa kuwa kitendo hicho cha askari huyo aliyekuwa na namba G2308 kimelifedhehesha Jeshi la Polisi baada ya video hiyo kusambaa mitandaoni akisema kwamba Gongo ni pombe safi akiipa jina la NIPA (New International Pure Alcohol), video ambayo imeonwa na watu wengi akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad