Chukua Hii..Ndoa ya Khalidi Aucho na Yanga iko Imara Sana, Ndio Mchezaji Bongo Anaishi Sehemu Ghali zaidi Kuliko Wote


Kama ambavyo niliripoti awali, Khalid Aucho ana mkataba wa miaka miwili na Yanga huku Kila kifungu cha mkataba kikitekelezwa vyema pande zote mbili

🔉Ni kweli Aucho alihitajika na klabu zote mbili ila kwake yeye haikuwa kuhusu mafanikio ya Klabu bali maslahi yake binafsi, Yanga walikidhi mahitaji yake ndipo akasaini nao

❌Taarifa za kuwa Simba watamsajili Aucho kwasasa sio za kweli na hakuna Kiongozi yoyote wa Simba aliejaribu kuwasiliana nae kwakuwa bado ana mkataba na Yanga

☑️Lolote linaweza kutokea kama matakwa ya kimkataba hayatotimizwa kama unavyofahamu wachezaji wa Uganda wana elimu kubwa juu ya mikataba, ila mpaka sasa Yanga wanatimiza kwa 100%

🔉Kwasasa Aucho hayupo dimbani kwakuwa anakamilisha program yake ya kurejea uwanjani chini ya Kocha wa Viungo, uwezekano Mkubwa atakuwepo kwenye derby

☑️Ndoa ya Aucho na Yanga ipo imara sana kwasasa Kila Mtu akimfurahia mwenzie

❗Aucho ni moja Kati ya wachezaji wachache sana wanaoishi sehemu ghali zaidi Jijini Dar Es Salaam, kwakuwa ni Professional na amehitaji kuishi maeneo yenye utulivu Mkubwa
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad