Cristiano Ronaldo na mpenzi wake Georgina Rodriguez Kupata Watoto Mapacha, Waweka Wazi Jinsia zao


Cristiano Ronaldo na mpenzi wake Georgina Rodriguez wametangaza jinsia za watoto wao mapacha ambao wanawatarajia kuwa ni wa Kike na wa Kiume. Ronaldo mwenye watoto Wanne, tayari ana watoto wengine mapacha wa Kike na wa Kiume (Eva na Mateo) aliowapata June mwaka 2017 kupitia njia ya mama mbadala.

Mtoto wake wa kwanza Cristiano Jr, alizaliwa June mwaka 2010 lakini hajawahi kumuweka wazi mama wa mtoto huyo kutokana makubaliano waliyoingia. Pamoja na Georgina Rodriguez wana mtoto mmoja wa Kike Alana Martina mwenye umri wa miaka 4.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad