Kuhusu Ishu ya Kumzuia Wawa Asiingie Uwanjani..Pablo Avunja Ukimya, Atoa Lawama

 


PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa kilichotokea kwenye mchezo wa ligi dhidi ya KMC ni kutoelewana na mwamuzi.

Juzi Pablo akiwa benchi alionekana kumzuia Pascal Wawa asiweze kuingia kuendelea kutimiza majukumu yake.


Kwenye mchezo huo ubao wa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ulisoma KMC 1-4 Simba na kuiwafanya mabingwa hao watetezi kusepa na pointi tatu.


Pablo amesema:”Suala hili halikuhitaji ufafanuzi lakini ni jambo ambalo limetokea katika mchezo wetu hasa katika upande wa mabadiliko.


“Jambo lililotokea naweza kusema ni kushindwa kuwa na mawasiliano mazuri na mwamuzi katika suala la mabadiliko lakini mambo mengine yanakwenda sawa.


“Sina tatizo na mchezaji Wawa kwa kuwa ni mchezaji mzuri na anatimiza majukumu yake,” amesema Pablo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad