Maneno ya Director Kenny Baada ya Kushinda Tuzo Marekani


Muongozaji wa video @director-kenny ameandika ujumbe huu wa shukrani mara baada ya kushinda Tuzo ya Muongozaji Bora wa Video kwenye Tuzo za African Entertainment Awards USA (AEAUSA) zilizotolewa usiku wa kuamkia leo.

Kenny kupitia ukurasa wake wa zinstagram ameandika ujumbe huu:

"Mungu amekuwa mkubwa sana kwangu amenibariki kwa tuzo yangu ya pili kubwa mwezi huu, yote ni baraka kutambulika katika kile unachofanya vizuri zaidi, napenda kusema asante bwana, nashukuru, na asante sana @aeausa kwa utambulisho huu una maana kubwa sana kwangu na kwa timu nzima ya @dk_limited.

"Asanteni sana wote waliochukua muda wao kunipigia kura, mbarikiwe Afrika Mashariki na Tanzania tuzo hii ni yetu sote!

Ukweli wako:

Mshindi wa Tuzo nyingi.

Direcror of The Year ! Tufanye kazi 2022"


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad