Mwanamke Ashikwa na Homa, Afariki Dunia Muda Mfupi Baada ya Kupokea Chanjo ya COVID-19



 
Mume wa Rhoda Mwikali John Matu Nderitu aliwaambia maafisa hao kuwa walitembelea hospitali ya Plainsview walikopata chanjo
Nderitu alisimulia kuwa waliondoka hospitalini baada ya kupewa chanjo ya Pfizer dhidi ya virusi vya corona
Mwikali alipata homa isiyo ya kawaida mara baada ya kuchanjwa na Nderitu akamkimbiza katika hospitali ya kaunti ndogo ya Ruiru
Mnamo Aprili 2021, mwanamke huyo ambaye alikuwa mjamzito alifariki dunia huko Uasin Gishu baada ya kuchanjwa na AstraZeneca
Mwanamke mwenye umri wa miaka 28 amefariki dunia baada ya kupokea chanjo ya COVID-19 huko Ruiru, kaunti ya Kiambu.

Kiambu: Mwanamke Ashikwa na Homa, Afariki Muda mfupi Baada ya Kupokea Chanjo ya COVID-19
Rhoda Mwikali alikuwa na mumewe wakati walipotembelea hospitali ya Plainsview kuchanjwa. Source: Facebook
Kwenye ripoti iliyowasilishwa katika kituo cha polisi cha Ruiru mnamo Alhamisi, Desemba 16, mumewe Rhoda Mwikali John Matu Nderitu aliwaambia maafisa hao kwamba walitembelea Hospitali ya Plainsview ambako walichanjwa.

Nderitu alisimulia kuwa wote wawili waliondoka hospitalini baada ya kupewa chanjo ya Pfizer dhidi ya virusi vya corona.

Hata hivyo, Mwikali alipatwa na homa isiyo ya kawaida mara baada ya kuchanjwa naye Nderitu akampeleka katika hospitali ya kaunti ndogo ya Ruiru kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.


 

Read also
Amason Kingi Abatilisha Msimamo na Kucheza Ngoma ya Raila, Atangaza Kumuunga

Lakini ilipofika mwendo wa saa moja alikuwa amekata kamba.

Maafisa wa polisi kutoka kituo cha Ruiru walitembelea hospitali hiyo na kuthibitisha kuwa Mwikali hakuwa na majeraha yoyote yaliyoonekana mwilini mwake.


Mwili wa marehemu ulipelekwa katika makafani ya hospitali ya General Kago kusubiri kufanyiwa upasuaji.

Mnamo Aprili 2021, mwanamke huyo ambaye alikuwa mjamzito alifariki dunia huko Uasin Gishu baada ya kuchanjwa na AstraZeneca.

Hata hivyo, Naibu Mkurugenzi wa Bodi ya Dawa na Sumu (PPB) Peter Ikamati alisema huenda mama huyo aliaga dunia kutokana na kuharibika kwa mimba aliyokuwa nayo na wala sio chanjo aliyopokea.

Kwingineko ni kuwa nchi kadhaa zilisitisha kutoa chanjo ya AstraZeneca COVID-19 kwa raia wao kutokana n hofu juu ya usalama na ufanisi.

Mnamo Jumatatu, Machi 15, Italia, Ufaransa na Ujerumani zilisema zitasitisha matumizi ya chanjo iliyotengenezwa na Oxford baada ya mataifa mengine kadhaa kuripoti kuhusu madhara yake.

Denmark na Norway zilisimamisha matumizi ya chanjo hiyo baada ya wagonjwa kadhaa kuganda damu, kuvuja damu na kupata idadi ndogo ya chembe chembe za damu baada ya kupokea chanjo hiyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad