Mwizi aiba chatu 15 wa kifalme Uingereza, msako mkali waanzishwa




Msako Mkali Wanzishwa Baada ya Mwizi Kuiba Chatu 15 wa Kifalme Uingereza

Kulingana na polisi, chatu hao wa kifalme walichukuliwa kutoka katika eneo la Hillmorton eneo la Rugby siku ya Jumamosi, Disemba 11, asubuhi.

BBC inaripoti kuwa mwizi huyo anaaminika kuwachukuwa wanyama hao na kuwapakia baada ya kuingia kwenye nyumba iliyoko Horne Close, kabla ya kupitia kwenye makaburi yaliyo karibu na kutoroka.

Kando na nyoka hao, polisi wanasema kuwa funguo na pesa pia viliibwa.


 
Wapelelezi wanasema chatu hao wana alama za kibinafsi ambazo zitawafanya kutambulika kwa urahisi iwapo watapatikana.

Inaripotiwa kuwa mhalifu huyo aliwachukua viumbe hao kupitia makaburi ya Watts Lane kisha kukimbia nao.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad