AFCON: Rapa Sarkodie karibia avunjeTV yake akitazama Morocco ikipiga Ghana




Video ya rapa maarufu raia wa Ghana Sarkodie akikosa utulivu akitazama mechi ya Black Stars' dhidi ya Morocco imeibuka
Rapa huyo anaonyeshwa akichachawika huku Black Stars wakilemewa na mabingwa wa Kaskazini mwa Afrika
Ghana ilipoteza mechi hiyo na kichapo cha 1-0, na kumvunja moyo mshindi huyo wa BET
Rapa maarufu raia wa Ghana, Michael Owusu Addo, almaarufu Sarkodie alikosa utulivu akitazama mechi ya Black Stars dhidi ya Morocco.

Karibia Rapa Sarkodie Avunje TV yake Akitazama Mechi ya Ghana Dhidi ya Morocco
Karibia Rapa Sarkodie Avunje TV yake Akitazama Mechi ya Ghana Dhidi ya Morocco.
Miamba hao wa Magharibi mwa Afrika walipata kichapo nyerezi kutoka kwa Atlas Lions of Morocco, baada ya bao la dakika ya lala salama kutoka kwa Sofiane Boufal na kuvunja moyo wa Waghana.

Katika video iliyopakiwa kwenye Twitter na SportsBrief.com, Sarkodie anaonyeshwa akikosa huku Black Stars wakilimwa na Morocco.

Sarkodie ambaye ni shabiki sugu wa Black Stars alikuwa na matumaini makubwa kabla ya mechi hiyo kuwa Ghana itatwaa ushindi.


 
"Penda usipende hisia hii ninayopata wakati nchi yangu inacheza," aliandika kwenye Twitter.

Mambo Bado Magumu kwa Aubameyang, Apatikana na Korona AFCON
Lakini Ghana ilipoteza mechi hiyo na kumvunja moyo mshindi huyo wa BET

Hata hivyo, timu hiyo inatazamiwa kufanya marekebisho itakapochuana na Gabon siku ya Ijumaa, Januari 14, 2021.

Black Stars wanasaka taji la tano la Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kushinda mara ya mwisho mnamo mwaka 1982.


Mvamizi wa zamani wa Southampton, Sofiane Boufal ndiye aliibuka shujaa katika mechi hiyo huku bao lake likiwafifisha Ghana katika mechi ya Kundi C katika kipute cha AFCON.

Makala ya mwaka huu ya AFCON yanaandaliwa nchini Cameroon.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad