Chama Aliamsha Moro Kabla ya Mchezo wa Leo Wakiwa Mazoezini, Apiga Pasi za Hatari



KIUNGO wa Simba, Clatous Chama ameanza kuwapa raha mashabiki wake mapema baada ya kupiga pasi zinazofika eneo husika.

Kocha wa Simba, Pablo Franco aliwapanga Chama, Rally Bwalya na Bernard Morrison kupiga mashuti nje ya 18, pia kupika kona.

Chama alifikisha mashuti yake eneo linalotakiwa, jambo ambalo liliwapa raha mastaa wenzake.

Pablo ni kama anamkabidhi majukumu Chama ya kupiga faulo, kwani amewatenga pembezoni mwa uwanja kupiga faulo, akiwa na Bwalya.


Kwa namna kocha anavyompa majukumu Chama ni dhahiri atampanga mchezo wa leo dhidi ya Mtibwa Sugar, ambao utapigwa Manungu.

Chama alipiga shuti kwa Hassan Dilunga ambaye alitokea katikakati la kundi la wachezaji wengine, huku Meddie Kagere,Chris Mugalu na Sakho wakikimbia kufunga.

Amewatenga mabeki Joash Onyango,Juma Kennedy na Inonga kuwawahi kina Kagere mbele.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad