Nay Mitego Afunguka Uhusiano Wake na Diamond Platnumz "Nimechoka Kuulizwa Kuhusu Mondi"




Ushkaji wa Diamond na Nay wa Mitego mara nyingi umekuwa ukisemekana kuingia dosari na hii inatokana na wawili hao kutoonekana pamoja kwa muda mrefu wala hakuna hata mmoja kati yao anaye support harakati za mwenzie, hawa ni washkaji ambao walikuwa wameiva sana na kufikia hatua ya kuachia kolabo mbili ambazo zilifanya poa sana way back ambazo ni Muziki gani na Mapenzi Pesa.

Ghafla ushkaji ukapungua na hadi leo haijulikani nani alimpunguza mwenzie, na Hakuna hata mmoja kati yao aliyewahi kukiri kuwa na ugomvi na mwenzake.

Hasa kupitia EFM Kwenye pindi la Empire hii leo Jan 13, Nay amedai katika maswali ambayo hapendi na amechoka kuyaongelea ni kuulizwa kama bado anaongea na Diamond,alicho kiongea ni kuwa ibaki tu kuwa kikubwa kila mmoja ana mishe zake na zinasonga.

Nay Amefunguka haya baada ya mtangazaji Jonijoo kutaka kujua kama bado wana ukaribu na Diamond kama ilivyokuwa zamani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad