Katiba ya Tanzania, Ibara ya 84(1) na 84(2) inatamka kuwa Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania anaweza kuwa mtu yeyote ambaye ana sifa za kuwa Mbunge (siyo lazima awe Mbunge).
Watu wenye madaraka kama Mawaziri, Naibu Waziri na wengine hawawezi kuchaguliwa kuwa Spika kwa mujibu wa katiba.
Aidha, kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Ibara ya 84(9) iwapo mtu asiye Mbunge akichaguliwa kuwa Spika wa Bunge atatakiwa kuapa Kiapo cha Uaminifu.