Wabongo Wamshukia Belle 9 , Ni Baada ya Kumsifia Zuchu, Diamond Ahusishwa


NIWARUDISHE NYUMA KIDOGO.
Siku tano zilizopita, Belle 9 alipost Clip kwenye Instagram yake, Clip hiyo anaonekana Zuchu akiimba wimbo wa Belle 9 "MASOGANGE"

Baada ya Belle 9 kupost clip hiyo, ilizuka sintofahamu, Watu hawakushangaa hiyo clip bali walishangaa Caption ambayo Belle 9 aliiandika chini ya video hio, jamaa aliandika "NI BARAKA KUONA STAR MKUBWA WA MUZIKI BARANI AFRIKA AKIENJOY MUZIKI WANGU, MUCH LOVE."

Watu wengi waliikosoa sana Caption ya Belle 9 huku wakidai kwamba jamaa kajishusha sana, inakuwaje kaanza muziki kitambo harafu anamuita mtoto mdogo(Zuchu) kwamba ni star mkubwa Africa. @hopetygatz najiuliza tu, hivi ni kosa kubwa msanii Kumsifia msanii mwenzake? Msanii kumsifia msanii mwenzake ni kujishusha?, Msanii hatakiwi kumsifia msanii mwenzake?

TUENDELEE
Jana Kupitia Refresh ya Wasafi Tv, Belle 9 amefunguka zaidi na amezidi kumsifia zuchu, kwamba ni msanii mkubwa sana Africa na hata nje ya Africa.

Wabongo hawajaacha lipite, wengi wamedai kwamba inakuwaje Belle 9 anamsifia Zuchu wakati Boss wa Zuchu(Mond) Mara nyingi huwa anahusishwa na Suala la Belle 9 kushuka kimuziki. @hopetygatz najiuliza, Hivi kama Belle 9 ana Bifu na Mond ndio Inabidi awachukie mpaka wasanii wa WCB?

Mi naona sio vibaya kabisa, Belle 9 kaongea ukweli, maana Zuchu ni msanii mkubwa sana kwasasa, Africa nzima inamjua, Imagine alivyotoa wimbo "CHECHE" kuna Media za nje ya Africa zilianza kumuita "Beyonce wa Africa" hii yote inaonesha ukubwa wa Zuchu Afrika na Nje Pia.

By @hopetytz

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad