Yanga yazidi kung'ara Ligi Kuu Tanzania bara



Vinara wa Ligi Kuu Tanzania bara timu ya Yanga imeendelea na wimbi la ushindi baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Tanzania Polisi mchezo uliopigwa katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid, jijini Arusha.

Shujaa wa Yanga ni winga mchachari aliyetokea benchi Dickson Ambundo aliwanyanyua washabiki wa Yanga dakika ya 64 akimalizia pasi ya Fiston Mayele.



Kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha Pointi 35 wakiwa wamecheza mechi 13 na kuwacha Simba kwa tofauti ya Pointi 10 ambao wapo nafasi ya pili wakiwa na Pointi 25 kwa mechi 12 walizocheza.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad