Young Lunya Afunguka Vesi Yake Kufutwa Katika Wimbo wa Conboi...Jay Mo Awekwa



Member wa kundi la Hip Hop nchini la OMG, Conboi ameachia Ep yake inayoitwa TRUE STORY ikibeba ngoma 4,na ngoma mojawapo inayopatikana kwenye EP hiyo inaitwa I made it akimshirikisha mkongwe wa Hip Hop nchini,Jay Mo Mchopanga.

Hasa kupitia Empire ya EFM,akijibu swali lililohusu kama ameisikiliza EP ya Conboi, Young Lunya ambaye pia ni OMG fam Amedai tusicho kijua ni kuwa ngoma zote tatu ukiacha ngoma ya nne kutoka kwenye EP hiyo, anazijua. Pia ametusanua kuwa wimbo wa I made it waliufanya muda kidogo na Conboi, ni wimbo ambao ulikuwa na Verse mbili tu, Yani verse yake (Lunya) na Conboi lakini amekuja kuisikiliza upya akakuta Verse yake imetolewa na ameshirikishwa Jay Mo.

Lunya amedai si kitu kibaya kufanya mabadiliko,lakini pia ameapreciate ukali wa Verse ya Mo Technique na kudai kuwa hana kinyongo chochote kwenye mabadiliko yaliyo fanyika kwenye wimbo huo.

Huu unakuwa muendelezo wa zile story zinazo semekana kuwa wana hawako poa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad