Khadija Kopa "Niliolewa Ndoa Nne na Zote Niliwaacha Mwenyewe Baada ya Kuona Hawaniridhishi"


MALKIA wa muziki wa Taarab Afrika, mzaliwa wa visiwa vya mashi ya karafuu, Zanzibar, Khadija Omary Kopa almaarufu Bi Khadija amekiri kuwa hadi sasa amewahi kuwa kwenye ndoa nne tofauti.

Bi Khadija ambaye ni mama ya staa wa Bongo Fleva, Zuhura Othman almaarufu Zuchu anasema kwamba, amekuwa akiwatema wanaume wake baada ya kuhisi haridhishwi nao.


“Kwa talaka zangu nne, sikuachwa, nimeachia mimi. Ningewaambia, wewe mwanaume huridhishi kaa ngozi ya futi, hebu nenda. Siyo eti sikuishi nao vizuri, nimeishi na waume zangu vizuri na bahati mbaya wanaondoka na wanapojutia na kutaka kurudi, mimi sina muda nao tena,” anasema Bi Khadija.

Bi Khadija anasema kuwa, kuna kipindi aliomba talaka yake ya kwanza baada ya mume wake kumuacha akiwa mjamzito na kupotea kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad