Mwanaziki Rihanna Afunguka "Nafurahia Ujauzito Wangu ndo Maana Naacha Tumbo Wazi"


Rihanna amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ujauzito wake, mwimbaji huyo alikuwa sehemu ya waliohudhuria red carpet kwenye event yake, Fenty Beauty Universe iliyofanyika Los Angeles Februari 11 mwaka huu.

Akizungumza na Jarida la PEOPLE, Rihanna alifunguka kuhusu changamoto za kuwa mwanamitindo wakati ukiwa mjamzito. "Napenda, Ninafurahia." alisema Riri. Badala ya kuficha tumbo, Rihanna amesema anafurahia na hana hofu ndio maana anaacha tumbo lake wazi.

Januari 31 mwaka huu Rihanna na A$AP Rocky walitangaza rasmi kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza pamoja kwa kuachia picha wakiwa matembezini mjini New York zilizomuonesha Riri akiwa mjamzito.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad