Viongozi wa CCM Waguswa na Hali ya Profesa Jay..Wamtembelea Hospitalini


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo leo alhamisi Februari 10, 2022 akiwa ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka wamemtembelea na kumjulia hali aliyekuwa Mbunge wa Mikumi mkoani Morogoro na Msanii Mkongwe wa Bongofleva Joseph Haule (Prof. Jay) alieyelazwa hospital ya Taifa Muhimbili akiendelea na matibabu.

"Tumemuona Ndugu yetu (Prof Jay) hali yake inazidi kuimarika, tumshukuru Mungu lakini niwashkuru madaktari kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kumhudumia, pamoja na mchango huu wa kuwezesha matatibu lakini kwa Niaba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan niwahakikishie tutaendelea kutoa kila aina ya ushirikiano katika kuhakikisha matibabu yanaendelea vyema huku tukiendelea kumuombea apone haraka" ——— Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad