Basata Wanarudia Kosa Kubwa Lililofanywa na EAT Awards Miaka Kadhaa iliyopita....Wasanii Kupeleka Kazi zao Ndo Uwepo Kwa Tuzo


Basata Imerudia Kosa Ambalo Tuzo za EATV Ilifanya Miaka Kadhaa la ili uwepo Kwa Tuzo lazima Uwasilishe Kazi zako, Hapo Ina Maana Kwamba Hata uwe na Hit Song Kubwa Kama hujapeleka Kazi basi wewe Tuzo sahau na ikapelekea Tuzo hizo kuonekana za Mchongo


Kosa Kubwa hapa Kwa Basata ni Kusema Watu Wasubmit Kazi hapo ndo Tatizo , Kama Tuzo za Taifa ni Bora mchague Watu kadhaa wanaojua Mziki na kuufatilia wakae Kama academy wapendekeze Wasanii Kwa Kila categories kulingana na Kazi zilizotoka Bila upendeleo wowote , hiii ya Kusema Watu watume Kazi zao ndo wawepo Kwenye Tuzo je Wasanii Wote wasipoleta Kazi inamaaana mtahairisha Tuzo au

Haya Sasa WCB na Wasanii wengine Ambao hawajapeleka Kazi Hawapo Katika Tuzo Hii inapelekea Tuzo kuonekana ni za Mchongo au hazifuati Uhalisia 

Ni wazi kabisa Baadhi ya Wasanii Kutoka WCB Kama Zuchu na Rayvanny wanastaili kuwepo Katika Vipengele hivyo

Kutoka Kwa Mdau

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad