Basi Lililosababisha Ajali Morogoro na Kuua Watu 22 Lilikuwa limetengenezwa Kwa Vifaa vya Ujenzi


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni amesema kuwa uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi kuhusu basi lililosababisha ajali wiki mbili zilizopita na kusababisha vifo vya watu 22 mkoani Morogoro, umeonesha kuwa lilitengenezwa kwa kutumia vifaa vya ujenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo wakati akitoa taarifa ya utafiti wa vyanzo vya ajali uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amesema uchunguzi umebainisha kuwa baadhi ya vifaa vilivyofungwa kama ‘ringboard’ hutumika kuweka zege kwenye ujenzi wa nyumba.

“Hizi ni Ringboard ambazo hutumika kuweka zege katika nyumba ndizo zimewekwa kwenye ‘chesis’ ya gari, na hizi ndizo zimekata viungo vya Watanzania,” amesema Masauni.

Waziri Masauni ameagiza kufanyika msako nchi nzima kwa magari yote yaliyofanyiwa hivyo, pia kumsaka mara moja mmiliki wa gari hilo pamoja na kiwanda kilichofunga kifaa hicho ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad