Kama Mwanaume Huna Ndevu Huko Taliban Basi na Kazi Huna

 


Kundi la Taliban limeagiza wafanyikazi wote wa serikali nchini Afghanistan kuwa na ndevu na kuzingatia kanuni za mavazi au kufukuzwa kazi kama wakishindwa kufanya hivyo.


Taarifa hiyo inasema wawakilishi kutoka Wizara ya Uenezi wa Utu wema wamefanya doria kwenye ofisi za serikali Jumatatu ili kuangalia kama watumishi wanafuata sheria mpya.


Wafanyakazi walikuwa wakielekezwa kutonyoa ndevu zao na kuvaa mavazi yenye urefu, suruali iliyolegea na kofia au kilemba.


Pia wameambiwa hawataweza kuingia ofisini bila ndevu na kutishiwa kupoteza kazi zao iwapo hawatafuata kanuni za mavazi zilizowekwa na utawala wa Kiislamu wenye msimamo mkali.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad