Kauli ya Rais Joe Biden - ''Marekani Tunasimama Na Ukraine, Putin Ametengwa"




Rais Joe Biden wa Marekani amesema madikteta ambao hawawajibishwi kutokana na uchokozi wao ndio wanaosababisha machafuko zaidi duniani.

Rais Joe Biden wa Marekani amesema madikteta ambao hawawajibishwi kutokana na uchokozi wao ndio wanaosababisha machafuko zaidi na kuongeza kuwa uvamizi wa rais Vladimir Putin wa Urusi nchini Ukraine ulikuwa ni wa kupangwa na wala haukuchochewa.

Rais Biden ameyasema hayo kwenye hotuba ya hali ya taifa aliyoitoa kwa bunge la Marekani. Biden amegusia pia umuhimu wa washirika wake wa Ulaya akisema muungano ulioanzishwa baada ya Vita vya Pili vya duniani ili kurejesha amani na ustahmilivu una umuhimu mkubwa pia katika kipindi hiki na kusema Putin alikosea sana kuamini angeweza kuugawanya ushirikiano wa NATO, kwa kukataa juhudi za kidiplomasia.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Annalena Baerbock kwa upande wake ametoa mwito kwa mataifa wanachama wa Umoja wa Mataifa kuunga mkono azimio la kulaani uvamizi huo wa Urusi, akisema ni wakati sasa wa kuchagua kati ya amani ama uvamizi, haki ama matakwa ya wenye nguvu, kuchukua hatua ama kufumbia macho. Amesema hayo kwenye mkutano wa dharura wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad