Wasanii Wachanga wa Nigeria ni Wakubwa Kuliko Wasanii Wakubwa wa Bongo Flava


Wasanii wachanga tokea nchini Nigeria kama Ruger,Rema,Fireboy DML,Ckay na Omah Lay wamekuwa ni mjadala mkubwa kwenye social Networks. Hii imekuja baada ya kuonekana wakifanya kolabo zaidi na wasanii wa Marekani. Mfano Rema ameonekana akila good time na Jason Derulo,lakini pia kuna Kolabo ambayo iko wazi na Rapa Lil Nas X.

Ijumaa hii Omah Lay anaachia kolabo yake na Justin Bieber inayoitwa Attention,msanii Fireboy DML pia yuko Marekani akiendelea na projects zake,baada ya kufanya kolabo na Ed Sheraan,kituo kifwatacho ni mwanamama Madonna.

Moja ya mjadala uliozuka Twitter ni kuwa,kwa trend hii, Wasanii wachanga wa Nigeria ni zaidi ya wasanii wakubwa wa Bongo Flava kama Diamond,Alikiba,Harmonize na Rayvanny. lakini pia tumeona Wasanii hawa wako interested kufanya kolabo na wasanii wa Nigeria,mfano Wiz Khalifa ametangaza kumshirikisha Wizkid kwenye goma lake, Miaka miwili Nyuma, Beyonce alimshirikisha WizKid kwenye goma lake,Drake pia.

Je unaungana na wanaoamini Wasanii wachanga wa Nigeria ni zaidi ya wasanii wakubwa wa Bongo Flava.?

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad