"Kuna Wanangu Walisema Nimejigeuza Rambo " - Rais Samia



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kwamba wakati akiwa nchini Marekani kwenye uzinduzi wa filamu ya The Royal Tour, aliona kwenye mitandao watu wakimsema kwamba badala ya kufanya kazi yeye amejigeuza kuwa Rambo anaigiza.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Aprili 28, 2022, Jijini Arusha, wakati wa uzinduzi wa filamu ya The Royal Tour, yenye lengo la kuutangaza utalii na vivutio vya utalii vilivyomo hapa nchini.

"Nimetumia siku 8 nje ya ofisi, lakini wakati nafanya hili jambo kuna wanangu nikawa nasoma kwenye mitandao huyu Mama badala ya kufanya kazi huko amejigeuza Rambo, Schwarzenegger anafanya filamu huko anaigiza, lakini nikasema ngoja tuone kitakachotoka," amesema Rais Samia
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad