Bodaboda Waliopora Wanusurika Kuchomwa Moto na Wananchi Mikocheni

 


Vijana wawili waliokuwa na bodaboda wamenusurika kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali, maeneo ya Mikocheni jijini Dar es Salaam, hii leo Julai 7, 2022, baada ya kupora pochi ya mwanamke na kukimbia na baadaye walizingirwa na kuanguka chini.

Taarifa zimeeleza kwamba vijana hao wameiba mbali kidogo na eneo Mikocheni, na kuanza kukimbia na hatimaye kujikuta mikononi mwa wananchi wenye hasira kali sana, ambapo pia walifanikiwa kujitaja majina yao kwamba ni Hassan na Michael.


Wananchi ambao hawakutaka kurekodiwa wala kujitambulisha majina yao, wamesema kwamba vijana hao wakati wanakimbizwa walianza kuchomoa panga kuwatishia raia waliokua wakiwakimbiza, kabla ya gari moja kuziba njia na kuwezesha vijana hao kuanguka chini na kujikuta mikononi mwa wananchi.





Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad