David Kafulila na Ally Hapi Watemwa Ukuu wa Mikoa...Chalamila Arudishwa


Ally Hapi na Kafulila ni miongoni mwa wakuu wa mikoa waliotemwa katika mkeka mpya huku wengine wapya wakiteuliwa mikoa mbalimbali na wengine kuendelea na kazi mikoa waliyokuwepo

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Albert Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera. Chalamila amewahi kuwa Mkuu wa Mikoa ya Mbeya na Mwanza

Mbali na Chalamila, Wakuu wa Mikoa wapya walioteuliwa ni pamoja na Peter Serukamba (Singida), Nurdin Babu (Kilimanjaro) na Fatma Mwasa (Morogoro)

Wengine ni Halima Dengego (Iringa), Dkt. Raphael Chegeni (Mara) na Dkt Yahaya Nawanda (Simiyu), Kanali Ahmed Abbas (Mtwara) na Kanali Laban Thomas (Ruvuma)

Wataapishwa Agosti 01, 2022
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad