Idadi ya washtakiwa wa mauaji Loliondo yaongezeka



 
Idadi ya washtakiwa katika kesi namba 11 ya  2022 dhidi Jamhuri wanaodaiwa  kufanya njama ya mauaji ya askari polisi katika pori tengefu  la loliondo  wilayani Ngorongoro imeongezeka  kutoka washtakiwa  25 na kufikia washtakiwa 27
Wakili wa serikali  Upendo Shemkole  mbele ya hakimu Mkazi Arusha anaesikiliza shauri hilo Heriet Mhenga  ameiambia mahakama kuwa mnamo tarehe tano mwezi wa saba mwaka huu, walileta mabadiliko katika hati ya mashtaka ya kuongeza washtakiwa wengine wawili ambao wanafikisha idadi ya washtakiwa ishirini na saba na kuiomba mahakama kumpa ridhaa ya kuwasomea tena  washtakiwa hao kesi inayowakabili kwa ujumla.

Maombi hayo yamepingwa  na jopo la mawakili wa upande wa utetezi wakiongozwa na wakili Jeremia, Mtebesya ambapo wameeleza kuwa   utaratibu uliotumika wa kubadilisha   hati hiyo  haujafuata sheria na taratibu..

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashataka mawili ambapo shtaka la kwanza linalowakabili ni kufanya  mauaji  ya askari polisi  namba G 4200  Koplo Galus Mwita mnamo June 10 mwaka huu  katika  eneo la Serie Ololosokwan Pamoja  na  kupanga njama za mauaji  kwa viongozi wa serikali waliokuwa wakifanya  zoezi la uwekwaji wa mipaka katika pori tengefu  la loliondo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad