Mfalme Zumaridi Amkataa Hakimu




Mwanza. Mshtakiwa namba moja katika kesi namba 10/2022, Diana Bundala maarufu Mfalme Zumaridi amemkataa hakimu anayesikiliza kesi yake, Monica Ndyekobora kwa kile alochodai kukosa imani naye.

Ombi la kumkataa hakimu huyo wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, limewasilishwa leo Julai 11, 2022 na Steven Kitale, wakili wa Mfalme Zumaridi wakati shauri hilo lilipoitwa kwa ajili ya kuendelea kusikiliza ushahidi.

Katika kesi hiyo Mfalme Zumaridi na wenzake nane wanakabiliwa na shtaka la kushambulia na kumsababishia majeraha Ofisa wa Jeshi la Polisi na kumzuia Ofisa Ustawi wa Jamii kutekeleza majukumu yake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad