Rasmi Simon Msuva Asaini Al Qadsiah



WINGA wa Kimataifa wa Tanzania, Simon Msuva amejiunga rasmi na klabu ya Al Qadsiah ya nchini Saudi Arabia.

Nyota huyo amejiunga na Klabu hiyo ya daraja la pili akitokea miamba ya Wydad Casablanca ambayo alikatisha nao mkataba.

Hatua hiyo imejiri baada ya Shirikisho la Soka Duniani FIFA kuiagiza klabu ya soka ya Wydad Casablanca ya Morocco kumlipa nyota huyo zaidi ya dola za kimarekani laki saba (zaidi ya Sh1.6 bilioni) kutokana na kitendo cha kushinda kesi ya madai aliyoifungua.

Msuva ambaye alikua amesaini mkataba wa miaka minne alilazimika kuusitisha mkataba wake Desemba mwaka jana kutokana na kuidai malimbikizo ya mishahara pamoja na pesa za usajili (signing fee).


Mbali na usajili huo ila pia klabu hiyo imenasa saini ya mshambuliaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Walter Bwalya (27) kwa uhamisho wa mkopo akitokea Al Ahly ya Misri.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad