Rwegasira ‘Apeta’ Unaibu Meya Kinondoni



Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, wamemchagua Joseph Rwegasira (Diwani wa Kata ya Makongo), kuwa Naibu Meya Mteule wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.



Rwegasira, anachukua nafasi iliyokuwa kishikiliwa na Heri Misinga ambaye muda wake utamalizika mwishoni mwa mwezi huu wa Julai, 2022.


Akiongea mara baada ya uchaguzi huo, Rwegasira amesema, “Ninawashukuru sana waheshimiwa madiwani kwa kuonyesha imani kubwa kwangu, naomba niwahakikishie kwa kushirikiana na Mstahiki meya tutahakikisha tunafanyakazi kwa pamoja ili kuwaletea maendeleo wananchi wetu ndani ya Manispaa yetu ya kinondoni.”

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad