Mwalimu Auwawa Akimsaidia Mtu Barabarani



Mwalimu wa Shule ya Msingi Mbaju Masasi mkoani Mtwara Mwanahawa Shaibu (50) ameuwa kwa kushambuliwa kwa mawe hadi kufa wakati akijaribu kumsaidia mtu aliyemkuta amelala barabarani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi (ACP) Nicodemus Katembo amesema mwalimu Mwanahawa kabla ya kukutwa na umauti alikuwa akitokea shuleni kwenda nyumbani Mbemba.

"Wakati akirudi nyumbani akiwa amepakiwa kwenye pikipiki alimkuta mtu akiwa amelala barabarani na aliposimama ili kujua mtu huyo amekutwa na matatizo gani hadi kufanya hivyo, ndipo aliposhambuliwa ghafla na mtu huyo kwa mawe bila sababu yoyote akaanguka na kupoteza maisha",amesema Kamanda Mbemba.

Amesema Jeshi la Polisi linaendelea kufanya uchunguzi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad