Raila Odinga Ajizolea Kura Nyingi Katika Wadi 2 Kwenye Ngome ya William Ruto




Mgombea urais wa Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga.
Mgombea urais wa Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga. Picha: Raila Odinga.
Raila alimbwaga Ruto katika wadi za Langas, Huruma zilizoko katika maeneo bunge ya Turbo na Kapseret mtawalia.

Kulingana na matokeo yaliyochapishwa kwenye Fomu 34A yanaashiria kwamba Raila kura nyingi katika wadi hizo ikilinganishwa na uchaguzi mkuu wa 2017.

Matokeo hayo yanaoonyesha kuwa Raila yuko kifua mbele katika wadi ya Huruma akizoa kura 11,843 dhidi ya Ruto aliyepata kura 5,749.


Didmus Barasa: Mbunge Mtoro Awashtua Wakenya Baada ya Kuonekana Mtandaoni
Katika wadi ya Huruma ambayo inajumuishwa makabila mengi ya jamii ya Waluhya, Waluo na Wakikuyu, wapiga kura waliosajiliwa ni 31,660.

Langas pia ina makabila mengi na wapiga kura 24, 763

Jemedari wa Raila atetea kiti chake bila jasho
Wakati huo huo Mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohamed alitetea kiti chake bila kutoa jasho akifanya kampeni mashinani.


Junet, ambaye pia ni katibu mkuu wa Muungano wa Azimio la Umoja, alijizolea kura 26,516 huku mpinzani wake Elias Okumu akipata kura 4,978 pekee.

Mbunge huyo mashuhuri alishinda kiti hicho bila kufanya kampeni huku mara nyingi akionekana akiandamana na mgombea urais wa Azimi Raila Odinga katika kila kampeni.

Didmus Barasa
Kwingineko, mbungeDidmus Barasa ameshinda kiti cha ubunge cha Kimilili siku moja baada ya kutoroka kufuatiaa madai ya kumpiga risasi msaidizi wa mpinzani wake Brian Khaemba.

Mbunge huyo mwenye ubishi alipata kura 26,000 huku Khaemba akipata kura 9,000
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad