Rappa Rosa Ree Awachimba Mkwara Marapa Wenzie Frida Amani na Chemical


Rappa Rosa Ree amewachimba mkwara marapa wenzie ambao ni Frida Amani na Chemical akiwataja kwamba wanahasira juu yake baada ya kujikita zaidi katika kile alichokiita kukazia nati.


"Badala mkazie nati mnakua na hasira, haya fukieni mashimo hii ni mazishi nitawazika!" ameandika Rosa Ree kupitia ukurasa wake wa Instagram.


Hata hivyo maoni mengi kwa mashabiki yanaonyesha kwamba huenda kuna ujio mpya kutoka kwa mkali huyo akitamba kuwa amewakalisha hao wenzake.


Itakumbukwa, Rosa Ree ameitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache tangu atangaze kufanya kazi na wasanii hao na ngoma hiyo itakuwepo kwenye album yake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad