Serikali yaongeza mishahara ya Walimu Shule za Msingi kwa 88%



Serikali nchini Rwanda, imeongeza mishahara ya Walimu wa shule za msingi, ambao sasa watapata nyongeza ya asilimia 88 ya mishahara yao kuanzia mwezi huu wa Agosti 2022, ikiwa ni sehemu ya motisha inayolenga kuboresha maisha yao.


Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya elimu ya nchi hiyo, iliyotolewa kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter Agosti 1, 2022 imesema chini ya marekebisho hayo mapya, walimu wa shule za upili pia watapata nyongeza ya malipo ya ongezeko la asilimia 40.


Aidha, taarifa hiyo ilibainisha kuwa mishahara halisi ya walio na cheti katika taaluma ya ualimu ambayo kwa sasa inaanzia 50,849 FRW (sawa na Tsh.114,472.22) na itapanda hadi Tsh. 215,221.86.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad