Baba Mzazi wa Ommy Dimpoz Atoa Neno Kuhusu Kazi yake ya Bajaji


Kupitia kipindi cha Clouds 360 cha Clouds Tv, Baba mzazi wa superstar Ommy Dimpoz, Mzee Faraj Nyembo amefunguka kuhusiana na kazi yake ya uendeshaji Bajaji huko Mjini Sumbawanga, akidai anashukuru anapata riziki kubwa ukilinganisha na kazi yake ya malori aliyokuwa akiifanya kabla.


"Maisha ya hapa Sumbawanga mazuri, baridi, chakula cha kutosha. Kazi yangu ni dereva wa magari makubwa lakini niliona Kwa sasa nipumzike maana nilikuwa nimeacha familia muda mrefu. Nimekaa Malawi, Zambia miaka miwili nimeamua nirudi nikae na familia. Nimenunua bajaj zangu mbili nimeamua nifanye shughuli zangu za bajaj kwa sababu zote ni usafirishaji tu"


"Kwa siku kwenye bajaj hapa Sumbawanga naweza kupata hadi Tshs Elfu 40 hadi 50 inategemea na hali ya usafiri. Maana muda mwingi nakuwa kwenye ibada.”


Mzee Nyembo amedai Kipato anacho kipata kupitia Bajaji kwakuwa anaendesha mwenyewe kina kidhi mahitaji yake na familia yake ukilinganisha na kazi ya malori aliyokuwa akisubiri kwa muda mrefu ujira wa laki mbili.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad