Fomu 34A hazikuhitilafiwa kwa njia yoyote - Jaji Martha Koome




Jaji wa mahakama ya upeo Martha Koome amepuuzilia mbali madai yaliyoibuliwa na upande wa malalamishi kwamba fomu 34A zilikuwa na mapungufu wakati wa kusukumwa kutoka vituo vya kupiga kura hadi IEBC.

 Akisoma uamuzi wa jopo la majaji saba wa mahakama hiyo, Koome alisema pia kwamba hata kama ripoti ya ukaguzi wa sajili ya wapiga kura ilitolewa siku 7 tu kelekea uchaguzi mkuu, sajili hiyo ilitumika bila mapungufu yoyote.


Akizungumzia madai ya uwepo wa mtu aliyekuwa katika seva za IEBC, jaji Koome alisema kwamba hakukuwa na ushahidi kwamba kulikuwepo na mtu kama huyo.

Alhamis wakili Julie Soweto aliibua madai kwamba kulikuwepo na mtu katika seva za IEBC kwa jina Jose Carmargo ambaye kulingana na yeye ndiye alibananga matokeo kwa upendeleo wa Ruto.

Vile vile jaji Koome alisema kwamba ushahidi uliowasilishwa na upande wa malalamishi haukuwa na uzito wa kuwafanya waamini kwamba teknolojia ya IEBC ilifeli.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad