Mbwana Samatta Aanza Moto Wake Baada ya Kurejea KRC Genk ya Ubelgiji...Atupia Goli la Ushindi


Mbwana Samatta Aanza Moto Wake Baada ya Kurejea KRC Genk ya Ubelgiji...Atupia Goli la Ushindi

Mtanzania Mbwana Samatta  anayecheza KRC Genk ya Ubelgiji leo amesaidia Timu yake kupata point tatu baada ya kufunga goli la ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Royale Union SG mchezo wa Ligi Kuu Ubelgiji.


Samatta aliingia akitokea benchi dakika ya 63 kuchukua nafasi ya Onuach wakati huo Genk wakiongoza 1-0 goli likifungwa na Paintsil dakika ya 15 kipindi cha kwanza na dakika ya 74 Royale kupitia kwa Lapoussin wakasawazisha.


Samatta sub yake ilizaa matunda licha ya kucheza kwa dakika 27 pekee ila dakika za nyongeza (90+2’), Samatta akafunga goli la ushindi na Timu kuondoka na alama zote tatu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad