Mlinzi Jeneza la Malkia Elizabeth Aanguka Ghafla

 


Mlinzi anayelinda jeneza la Hayati Malkia Elizabeth II, ameanguka ghafla wakati wa maandalizi ya kuagwa kwa mwili wa Kiongozi huyo aliyeitawala Uingereza kwa muda mrefu (miaka 70), kwenye ukumbi wa Westminster Hall jijini London.


Tukio hilo, limetokea wakati raia wa Uingereza wakiendelea na zoezi la kuaga mwili wa Malkia huyo aliyefariki hivi karibuni, ambapo chanzo cha kuanguka kwa mlinzi huyo hakikuweza kufahamika mara moja.

Mara baada ya kuanguka kwa mlinzi huyo, Televisheni ambayo ilikuwa ikirusha matangazo hayo mubashara ilisitisha matangazo wakati mlinzi huyo akipatiwa matibabu ya dharura.


Jeneza la Hayati Malkia Elizabeth II, linalindwa kikosi maalum kinachofahamika kama Sovereign’s Bodyguard.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad