Mwanajeshi Ajinyonga na Mkanda wa Jeshi, Aacha Ujumbe kwa Mama na Mke Wake




Dodoma. Askari wa Jeshi la Anga, William Giriango (40) amejinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali aliokuwa ameutundika katika nondo ya dirisha katika chumba cha kulala wageni, Mtaa za Hazina jijini Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martine Ortieno akizungumzia tukio hilo leo Jumatano, Septemba 7, 2022 amesema lilitokea jana Jumanne kwa askari huyo wa makao makuu jijini Dar es Salaam kujinyonga.

Amesema baada ya kupekuliwa marehemu alikutwa ameandika ujumbe mbalimbali katika karatasi.

Ujumbe huo ni ‘kwako mama Derick, nisamehe sana kwa maamuzi haya maisha kwangu hayana maana tena, nisamehe sana, nimejitahidi nimeshindwa, naomba uwatunze watoto wetu.”


Kamanda Otieno amesema ujumbe mwingine aliouandika marehemu ni “mama yangu nisamehe sana nakuomba.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad