Makocha Simba waomba kazi Dodoma Jiji yumo Medo




Dodoma. Waliowahi kuwa makocha wa klabu ya Simba,Dyran Kerry na Goran Kopunovic  ni sehemu  ya zaidi ya makocha 20 walioomba kibarua cha kuifundisha  Dodoma Jiji.

Mbali na makocha hao pia aliyewahi kuwa kocha wa Coastal Union Melis Medo naye anatwaja kuomba nafasi hiyo.

Kerry  amewahi kuinoa Simba msimu wa 2015-2016 huku   Kopunovic akiifundisha msimu  wa 2014-2015.

Mapema leo  uongozi wa Dodoma Jiji umetangaza  kuachana  na benchi zima  la ufundi la klabu hiyo  lilokuwa likiongozwa na Masoud Djuma na  sababu zikitajwa ni matokeo mabovu ya klabu hiyo.


Mbali na Djuma wengine waliotupiwa virago ni kocha msaidizi Mohammed Muya na kocha wa makipa,Adam Meja ambaye inadaiwa amejiunga na Simba Queens.

Februari 24 mwaka huu uongozi wa klabu hiyo ulimtangaza Djuma kuiongoza timu  hiyo akichukua nafasi ya Mbwana Makata ambaye aliyetupiwa  virago.

Kocha huyo ameiongoza klabu hiyo katika michezo 21 ikifungwa 10, sare mitano na kushinda sita.


Mchezo wake wa kwanza ulikuwa  dhidi ya Ruvu Shooting mtanange ulifanyika  Mabatini mkoani Pwani  na timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1 huku wa mwisho ukiwa dhidi ya Simba ambao ulimazika kwa kukubali kichapo cha mabao 3-0.

Msimu huu ameiongoza klabu hiyo katika michezo sita na imeshinda mechi  moja  na kutoa sare miwili huku ikipoteza michezo  mitatu na katika msimamo inashika  nafasi ya 14.

Akizungumza na Mwanaspoti leo Oktoba 10 Jijini hapa,Kaimu Katibu  Mkuu wa timu hiyo,Fredrick  Mwakisambwe  amesema zaidi ya makocha 20 wameomba nafasi hiyo wakiwemo makocha hao.

“Makocha walioomba ni wengi mno hata makocha wa zamani wa Simba wameomba.Yule  aliyekuwa Coastal Union Medo nae ameomba  pamoja na wazawa wengi, tunapitia CV zao na tutamtangaza kocha ambaye tutakuwa naye,”amesema Mwakisambwa.


Hata hivyo Mwanaspoti inajua tayari uongozi wa klabu hiyo unakaribia kumtangaza  Medo kuchukua nafasi ya Djuma.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad