Mwanafunzi Ajinyonga Mwalimu Kumtaka Anyoe Nywele


Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Langalanga, Shamamcy Wanjiru (17) amekutwa amejinyonga ndani ya nyumba yao eneo la Kaloleni Estate nchini Kenya baada ya kupewa agizo na shule kunyoa nywele zake.

Kulingana na bibi yake, Jane Wairimu, marehemu alikuwa amepewa adhabu hiyo na mwalimu wake baada ya yeye na wanafunzi wengine kukutwa wakiwa wanachana nywele zao shuleni.

Inadaiwa, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Bi Rufina Nkonge alimrudisha nyumbani kwa mlezi wake kwa nia ya kujadili suala hilo baada ya kushindwa kunyoa nywele zake pamoja na barua iliyomtaka mlezi wake afike shuleni mnamo Septemba 28, 2022 ili kujadili suala la binti huyo kunyoa nywele zake.

Zaidi tembelea swahilitimes.co.tz

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad