Haji Manara "Kuwafananiaha Makipa Wetu na Diarra ni Kujitafutia Dhambi"


“Ni kweli tuna Makipa bora sana kwenye Ligi kuu yetu ila kuwafananiaha Makipa wetu na Diarra ni kujitafutia dhambi kama za kuzini tu.

Huyu hadaki tu kizamani kama Watangazaji wetu wa wakati ule walivyokuwa wakitangaza,, kadaka kama Nyani.

Huyu ni kipa wa kisasa,, anafanya saves,, ile kurukia mpira kama Nyani ni uzamani,, kazi ya kipa wa kileo ni kuzuia lango lake mpira usingie,, sio kuruka ruka hovyo.

Kisha anawazidi wote chini, yeye ni Sweeper kisha Boll Control yake ni ya makipa wa hadhi ya kidunia,, anaanzisha mwenyewe mashambulizi, tena sio Kwa kurusha ili kuwahi counter attacks, anapasia kwa Miguu yake.

Kubwa ni Commanding Goalkeeper, ni kiongozi ndani ya Uwanja,, Kiukweli ubora wake ni mkubwa kuliko maradufu ya wenzake, kawaacha mbali mno.

Yeye yupo Makka wenzake wapo Nantumbo… ✍🏼
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad