Uongozi wa Klabu ya Simba Wamkataa Kocha Aliyekamatwa na Madawa ya Kulevya


Uongozi wa Klabu ya Simba unaujulisha umma kuwa aliyekuwa Kocha wa makipa Muharami Said Mohammed maarufu ‘Shilton’ , hakuwa muajiriwa wa klabu hiyo na wala hakuwa na mkataba na Simba.

Simba ilimuomba Muharami kuwanoa makipa wake kwa muda kwa mwezi mmoja, wakati huo klabu ikiendelea kutafuta Kocha wa kudumu.

Kwa mantiki hiyo klabu haihusiki na tuhuma zinazomkabili Kocha huyo na klabu iko tayari kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika pindi itakapohitajika kwa maslahi ya Taifa.

Uongozi wa Simba unawaomba mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kwani hakuna athari yeyote kwa klabu kutokana na kadhia iliyomkumba Kocha huyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad