Comment ya mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini @masterjtz imezua gumzo huko kenya baada ya kudai kuwa mwanamuziki kutoka tanzania @diamondplatnumz ameingiza pesa nyingi katika show moja kuliko A-list ya wasanii wote wa kenya wakiungana.
Master J ambae ni miongoni mwa judges wakongwe wa shindano la kutafuta vipaji nchini Bongo Star Search amemjibu shabiki huyo kutoka kenya ambae amedai kuwa wasanii wa chini wa kenya wanaingiza hela nyingi kuliko wasanii wa Tanzania.