TANZIA: Mchezaji wa Timu ya Vijana U-17 ya Singida Big Stars Mohammed Amefariki Dunia Uwanjani





Dodoma. Mchezaji wa timu ya vijana U 17 ya Singida Big Stars Mohammed maarufu Banda amefariki mazoezi mara baada ya kugongana na mchezaji mwenzake wakati wakigombea mpira wa juu.

Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Singida (Sirefa), Hamis Kitila amethibitisha kutokea kwa kifo hicho.

Mwenyekiti huyo amesema  mchezaji huyo amefariki leo asubuhi wakati timu ya U17  ikifanya mazoezi katika uwanja wa Magereza mkoani Singida.


"Ni kweli walikuwa kwenye mazoezi asubuhi  jina la marehemu  anaitwa Mohammed hili Banda ni la utani lakini anajulikana zaidi kwa jina hilo," amesema Kitila.

Kitila amesema kwa sasa vikao vinaendelea na watatoa utaratibu baadae nini kinachofuata.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad